|
Sera
ya Lishe
Jitihada za serikali za kuinua kiwango cha ubora wa huduma za afya na
lishe katika jamii zimezingatia mambo muhimu kama vile utoaji wa
miongozo ya kisiasa, kupitisha sera mbalimbali, kubuni na kuchukua hatua
mahususi zinazolenga katika kuinua hali ya lishe. Sera na hatua hizo
zilianza kubuniwa na kutekelezwa mara baada ya kupatikana kwa uhuru
mwaka 1961 na kuimarika zaidi baada ya Azimio la Arusha la mwaka 1967.
[bonyeza
hapa]

Mwongozo wa Kitaifa Kuhusu Matunzo na Huduma za Lishe kwa Watu Wanaoishi
na Virusi Vya Ukimwi na Wenye Ukimwi.
Hivi sasa tatizo la maambukizo ya virusi vya UKIMWI duniani limekuwa
kubwa kuliko ilivyofikiriwa miaka ya nyuma. Nchini Tanzania kiwango cha
maambukizo kiko juu, yaani asilimia 9.6 kwa watu wazima.[bonyeza
hapa]
Mwongozo
wa Ulaji Bora kwa Watu Wanaoishi na Virusi Vya Ukimwi na Wenye Ukimwi
Tatizo la VVU/UKIMWI linaendelea kuwa tishio kwa maisha ya
binadamu. Pamoja na jitihada mbalimbali za kitabibu, imeonekana kuwa
watu wengi wanaoishi na virusi vya UKIMWI (VVU) au UKIMWI huathirika au
hupoteza maisha yao mapema zaidi kwa kukosa lishe bora. [bonyeza
hapa] |
|